Yeriko
Yeriko (kwa Kiebrania יְרִיחוֹ, kwa Kiarabu أريحا, maana yake "wenye kunukia") ni mji wa kale sana, ulioanzishwa miaka 9000 hivi KK karibu na mto Yordani.
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/c4/Entering_jericho_south.jpg/300px-Entering_jericho_south.jpg)
Upekee wake
Umaarufu wake unatokana na kuwa chini ya usawa wa bahari kuliko miji yote duniani.
Unasadikiwa pia kuwa mmojawapo kati ya miji ya zamani zaidi kukaliwa mfululizo hadi leo.[3][4][5]
Akiolojia imekuta chini ya ardhi zaidi ya miji 20 iliyojengwa kwa nyakati tofauti mahali pale, kuanzia miaka 11,000 iliyopita.[6]
Katika Biblia
Katika Biblia unatajwa kama "Mji wa Mitende": chemchemi mbalimbali ndani na kandokando yake zilivuta binadamu tangu milenia nyingi.[7]
Katika Agano la Kale unatajwa kwa namna ya pekee kuhusiana na Yoshua kuingiza Waisraeli waliotoka Misri katika nchi ya Kanaani kwa kuvuka mto Yordani mkabala wa Yeriko na kuuteka kwa maandamano ya ibada (Yos 6) kabla ya miji mingine yoyote.
Katika Agano Jipya unatajwa kuhusiana na Yesu ambaye huko alimuongoa mtozaushuru tajiri Zakayo (Luk 19) na kumponya kipofu ombaomba Bartimayo (Mk 10).
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
- Jericho (Ariha) - History Archived 10 Februari 2007 at the Wayback Machine. Studium Biblicum Franciscum - Jerusalem.
- Telepherique & Sultan Tourist Center
- Jericho Municipality Official Website Archived 9 Agosti 2014 at the Wayback Machine.
- Jericho Municipality Official Website Historical site Archived 17 Septemba 2008 at the Wayback Machine.
- Resources on Biblical Archaeology Archived 21 Septemba 2019 at the Wayback Machine.
- Archaeological History of Jericho Archived 23 Mei 2007 at the Wayback Machine.
- Jericho: Tel es-Sultan Archived 13 Oktoba 2008 at the Wayback Machine.
- The walls of Jericho fell in 1550 BCE