Xiaomi

Kampuni ya Xiaomi (ɕi̯ɑomi;[1] (Kichina)), inajulikana kawaida kama ximi na imesajiliwa kama Xiaomi Inc. Ni kampuni inayojikita na utengenezaji wa vifaa mbalimbali vya simu, na vifaa vya nyumbani. Ni mtengenezaji wa pili kwa ukubwa wa simu ya mkononi duniani, nyuma ya Samsung,[2] ambayo kwa kiasi kikubwa inatumia mfumo wa Android. Kampuni hiyo inashika nafasi ya 338 na ni kampuni changa.[3][4]

[5] Ifikapo 2015, ilikuwa inaendeleza anuwai kubwa ya elektroniki za watumiaji.[6] Mwaka 2020, kampuni hiyo iliuza simu milioni 146.3 na UI yake ya simu ya mkononi ya MIUI ina zaidi ya watumiaji milioni 500 kila mwezi.[7] Kufikia 2023, Xiaomi ndiyo muuzaji wa tatu kwa ukubwa wa simu za mkononi ulimwenguni, na sehemu ya soko ya karibu 12%, kulingana na Counterpoint.[8] Uwepo wake ulisababisha baadhi ya watu kuiita Xiaomi "Apple ya China".[9] Imekuja na anuwai yake ya vitu vya kuvaa. [10] Pia ni mtengenezaji mkubwa wa vifaa ikiwa ni pamoja na televisheni, torchi, ndege isiyokuwa na rubani, na kifaa cha kusafisha hewa kutumia mfumo wake wa Internet of things na Xiaomi Smart Home.

[11][12][13][14]

Listi ya baadhi ya simu za Xiaomi

  • Xiaomi Mi 11: Ilizinduliwa mwaka 2020, ina kamera bora na utendaji wa hali ya juu.
  • Xiaomi Mi 11 Pro: Toleo la kuboreshwa la Mi 11 na sifa zaidi za kamera na utendaji.
  • Xiaomi Mi 11 Ultra: Simu yenye sifa za hali ya juu, hasa kwenye kamera na skrini.
  • Xiaomi Mi 10T Pro: Inajulikana kwa kamera yake bora na uwezo wa 5G.
  • Xiaomi Redmi Note 10: Simu ya bei nafuu na sifa nzuri za kamera.
  • Xiaomi Redmi Note 9 Pro: Inatoa utendaji mzuri kwa bei nafuu.
  • Xiaomi Poco X3: Simu yenye bei nafuu na utendaji mzuri.
  • Xiaomi Mi Mix 4: Inajulikana kwa muundo wake wa kuvutia na sifa za hali ya juu.
  • Xiaomi Redmi K40: Simu yenye bei nafuu na kamera bora.
  • Xiaomi Black Shark 4 Pro: Inalenga watumiaji wa michezo na ina utendaji wa hali ya juu.

Marejeo

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Xiaomi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.