Visiwa vya Marshall

Visiwa vya Marshall ni nchi ya visiwani ya Mikronesia katika Pasifiki ya magharibi.

Aolepān Aorōkin M̧ajeļ
Republic of the Marshall Islands
Jamhuri ya Visiwa vya Marshall
Bendera ya Marshall IslandsNembo ya Marshall Islands
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa: "Jepilpilin ke ejukaan"
Wimbo wa taifa: Forever Marshall Islands
Lokeshen ya Marshall Islands
Mji mkuuMajuro
7°7′ N 171°4′ E
Mji mkubwa nchiniMajuro
Lugha rasmiMarshallese, Kiingereza
Serikali
Rais

Hilda Heine
Uhuru
kutoka Marekani

21 Oktoba 1986
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
181 km² (ya 213)
‘‘(kidogo sana)’’
Idadi ya watu
 - Julai 2009 kadirio
 - 2021 sensa
 - Msongamano wa watu
 
68,000 (ya 205)
42,418
233/km² (ya 28)
FedhaUS Dollar (USD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+12)
(UTC)
Intaneti TLD.mh
Kodi ya simu+692

-


Nchi jirani katika bahari ni Nauru, Kiribati, Shirikisho la Mikronesia na eneo la Marekani la Kisiwa cha Wake.

Atolli ya Majuro inashika nafasi ya mji mkuu.

Jiografia

Eneo la visiwa vya Marshall ni safu mbili za visiwa au atolli zinazoelea sambamba:

Kwa jumla kuna visiwa na vipande vya atolli 1,150 katika eneo la bahari la km² 1,900,000.

Historia

Jina limetokana na nahodha Mwingereza John Marshall aliyetembelea eneo hili mwaka 1788 na kulichora katika ramani. Ingawa visiwa vilikaliwa tayari tangu karne nyingi na watu kutoka Mikronesia lakini jina la Kizungu limebaki kwa ajili ya jumla ya visiwa.

Mwisho wa karne ya 19 Ujerumani ulianzisha ukoloni juu ya visiwa ukaviunganisha kiutawala na Guinea Mpya ya Kijerumani.

Katika vita kuu ya kwanza ya dunia vilitwaliwa na Japani iliyoendelea kutawala visiwa kama eneo lindwa kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa.

Baada ya vita kuu ya pili ya dunia vilikuwa chini ya Marekani.

Mwaka 1979 visiwa vimepata madaraka ya kujitawala na hatimaye kupokea uhuru kufuatana na azimio la Umoja wa Mataifa mwaka 1990.

Majaribio ya kinyuklia

Kuanzia mwaka 1946 Marekani ilitumia visiwa kwa ajili ya majaribio ya mabomu ya nyuklia.

Hadi mwaka 1958 ilitokea milipuko 6,913 kwenye atolli za Bikini na Eniwetok. Hadi leo kuna wakazi wa visiwa wanavyoteswa na maradhi yaliyosababishwa na mnururisho wa mabomu haya. Bikini haitawezekana kukaliwa na watu kabla ya mwaka 2050, Eniwetok haifai kwa makazi ya binadamu kwa miaka 24,000 inayokuja.

Watu

Wakazi ni 68,000, wengi wakiwa wametokana na wenyeji wa kwanza.

Upande wa dini, wengi ni Wakristo, hasa Wakalvini (51.5%), Wapentekoste, Wakatoliki, mbali ya Wamormoni (8.3%).

Tazama pia

Viungo vya nje

WikiMedia Commons


Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.