Ugiriki

nchi katika Ulaya Kusini-Mashariki

Ugiriki (pia: Uyunani; kwa Kigiriki cha kisasa: Ελλάδα, Ellada, au Ελλάς, Ellas) ni nchi ya Ulaya Kusini-Mashariki iliyopo kusini mwa rasi ya Balkani.

Ελληνική Δημοκρατία
Ellinikí Dimokratía

Demokrasia ya Ugiriki
Bendera ya GreeceNembo ya Greece
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa: Ελευθερία ή Θάνατος
(Eleftheria i thanatos - "Uhuru au mauti")
Wimbo wa taifa: Ύμνος εις την Ελευθερίαν - "Wimbo la Uhuru"
Lokeshen ya Greece
Mji mkuuAthens
38°00′ N 23°43′ E
Mji mkubwa nchiniAthens
Lugha rasmiKigiriki
Serikali
Rais
Waziri Mkuu
Jamhuri
Katerina Sakellaropoulou (Κατερίνα Σακελλαροπούλου)
Kyriakos Mitsotakis (Κυριάκος Μητσοτάκης)
Uhuru
Ilitangazwa
Ilitambuliwa

25 Machi 1821
1829
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
131,957 km² (ya 95)
1.51
Idadi ya watu
 - 2021 kadirio
 - 2012 sensa
 - Msongamano wa watu
 
10,678,632 (ya 85)
10,816,286
77/km² (ya 120)
FedhaEuro (€)2 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
EET (UTC+2)
EEST (UTC+3)
Intaneti TLD.gr 3
Kodi ya simu+30

-

1 Wananchi walikataza kurudi kwa ufalme tar. 8 Desemba 1974.
2 Prior to 2001: Greek Drachma.


Imepakana na Albania, Masedonia Kaskazini, Bulgaria na Uturuki. Upande wa kusini-magharibi na kusini-mashariki kuna pwani ndefu kwenye Bahari ya Mediteranea.

Jiografia

Kijiografia huwa na sehemu za Ugiriki bara, rasi ya Peloponesi upande wa kusini inayounganishwa kwa shingo ya nchi nyembamba, halafu visiwa vingi upande wa Bahari ya Aegean, Bahari ya Adria na kwenye Mediteranea yenyewe. Visiwa vikubwa zaidi ni Kreta, Euboea, Lesbo na Rhodos.

Historia

Parthenon, katika Akropoli ya Athens, ni kielelezo cha Ugiriki wa Kale.

Ugiriki ni nchi yenye historia ndefu na maarufu sana, hata inaitwa "nchi mama ya Ulaya" na kitovu cha Ustaarabu wa magharibi, kwa sababu ndipo vilipoanza demokrasia, falsafa ya magharibi, fasihi ya magharibi, historiografia, sayansi ya siasa, tafiti za sayansi na hisabati, tamthilia na michezo ya Olimpiki.

Ugiriki ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 1981.

Watu

Lugha ya Kigiriki inaendelea kuandikwa kwa Alfabeti ya Kigiriki inayotumiwa tangu miaka 3000 iliyopita, lakini lugha yenyewe imebadilika. Wagiriki wa leo hawaelewi tena Kigiriki cha Kale moja kwa moja.

Wakazi wengi wanafuata dini ya Ukristo (93%), hasa katika Kanisa la Kiorthodoksi la Kigiriki (90%), halafu Waprotestanti na Wakatoliki. 2% ni Waislamu.

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje


Nchi za Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ugiriki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.