Simon Nkoli

mwanaharakati (1957-1998)

Simon Tseko Nkoli (26 Novemba 1957 - 30 Novemba 1998) alikuwa mpinzani wa ubaguzi wa rangi, mdai haki za mashoga na mwanaharakati wa UKIMWI wa Afrika Kusini.

Mwanaharakati shoga Simon Nkoli

Maisha

Nkoli alizaliwa Soweto katika familia inayozungumza SeSotho. Alikulia na familia yake kwenye shamba huko Free State, baadaye ilihamia Sebokeng. Nkoli alikuwa mwanaharakati wa vijana dhidi ya ubaguzi wa rangi, akiwa na Baraza la Wanafunzi wa Afrika Kusini (COSAS) na United Democratic Front.

Mnamo mwaka 1983, alijiunga na Chama cha Mashoga cha Afrika Kusini (kilichounganisha hasa Wazungu), kisha akaunda Kikundi cha Jumamosi, kikundi cha kwanza cha mashoga Weusi barani Afrika.

Nkoli alihutubia mikutano ya hadhara ya kuunga mkono kugomewa kwa kodi za nyumba katika mitaa ya watu weusi. Mnamo mwaka 1984 alikamatwa akashtakiwa kutenda uhaini na kutishiwa adhabu ya mauti pamoja na viongozi wengine 21 wa kisiasa katika Kesi ya Uhaini ya Delmas, akiwa na Popo Molefe na Patrick Lekota, ambao wote kwa pamoja wanajulikana kama Delmas 22. Aliachiliwa huru na kutolewa gerezani mwaka 1988. Kwa kuwa wazi kuliko hali yake ya ushoga akiwa mfungwa, alisaidia kubadilisha mtazamo wa African National Congress kuhusu haki za mashoga.

Alianzisha Shirika la Mashoga na Wasagaji la Witwatersrand (GLOW) mwaka 1988.[1] Pamoja na mwanaharakati wa LGBT, Beverley Palesa Ditsie, aliandaa onyesho la kwanza lijulikanalo kama gwaride la kujivunia nchini Afrika Kusini lililofanyika mnamo 1990.[2] Alisafiri sana na alipewa tuzo kadhaa za haki za binadamu huko Ulaya na Amerika Kaskazini. Alikuwa mwanachama wa bodi ya Chama cha Kimataifa cha Washoga na Wasagaji, akiwakilisha eneo la Afrika.

Alikuwa mmoja wa wanaharakati wa kwanza wa ushoga kukutana na Rais Nelson Mandela mwaka 1994. Alishiriki katika kampeni ya kuingiza kinga dhidi ya ubaguzi wa kijinsia katika Orodha ya Haki za Binadamu kwenye Katiba ya Afrika Kusini ya 1994. Alishiriki pia katika kampeni ya kufuta sheria dhidi ya ulawiti iliyofanyika Mei 1998.

Baada ya kuwa kati ya mashoga Waafrika wa kwanza waliokiri hadharani kuambukizwa VVU, alianzisha kikundi Positive African Men (Wanaume Waathirika wa Kiafrika) mjini Johannesburg. Aliishi na VVU kwa karibu miaka 12, na miaka minne ya mwisho alikuwa akiumwa vibaya, akiwa na vipindi vya kujisikia nafuu. Alifariki dunia kwa UKIMWI mwaka 1998 huko Johannesburg.

Kuna siku ya kumbukumbu ya Simon Nkoli huko San Francisco, Marekani. Alifungua Michezo ya Mashoga ya kwanza huko New York akapewa na meya David Dinkins tuzo ya heshima ya jiji hilo. Mwaka 1996 Nkoli alipokea Tuzo ya Stonewall katika Royal Albert Hall huko London.

Msanii wa filamu wa Kanada John Greyson alitengeneza filamu fupi kuhusu Nkoli iliyopewa jina la "A Moffie Called Simon" mwaka 1987.[3] Nkoli alikuwa mhusika katika tamthilia ya Robert Colman wa 2003, "Your Loving Simon" na filamu ya Beverley Ditsie ya 2002 "Simon & I".[4] Filamu ya John Greyson ya 2009 "Fig Trees", maandishi / opera ya mseto ni pamoja na kumbukumbu ya uanaharakati wa Nkoli.[5]

Marejeo

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Simon Nkoli kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.