Nana Ama Dokua Asiamah Adjei

Mwanasiasa wa Ghana


Nana Dokua Asiamah Adjei (amezaliwa 24 Julai 1982) ni mwanasiasa wa Ghana na mbunge wa Jimbo la Akuapem Kaskazini Mashariki mwa Ghana. Ni mwanachama wa New Patriotic Party ambaye kwa sasa ni Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda wa Ghana. Hapo awali alikuwa Naibu Waziri wa Habari.[1][2][3][4]

Nana Dokua Asiamah Adjei

Mbunge wa Ghana wa Akuapem Kaskazini Aliyepo madarakani
Amezaliwa24 Julai 1982
Ghana
NchiGhana
Kazi yakemwanasiasa

Maisha ya utotoni na elimu

Adjei alizaliwa tarehe 24 Julai 1982 na Nana Osae Nyampong IV na Aforo Asiamah-Adjei huko Akropong, Mkoa wa Mashariki. Alipata elimu yake ya msingi na shule ya upili katika Alsyd Academy na shule ya Upili ya St. Roses mtawalia. Ana shahada ya kwanza katika Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Ghana na shahada ya uzamili katika Logistiki na Ugavi kutoka Chuo Kikuu cha Exter nchini Uingereza.[5][6][1]

Maisha binafsi

Adjei ameolewa na Charles Bissue. Kwa upande wa dini yeye amejitambulisha kuwa ni Mkristo.[6]

Marejeo

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nana Ama Dokua Asiamah Adjei kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.