Mkesha-maji
Mkesha-maji | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mkesha-maji wa Ulaya | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Spishi 5:
|
Mikesha-maji ni ndege wadogo kiasi wa familia Cinclidae wafananao na mikesha wadogo. Katika Afrika wanatokea Milima ya Atlas huko Maroko. Wana mkia mfupi na mabawa mafupi yenye nguvu. Ndege hawa hutafuta chakula majini na waweza kuingia maji wakizama kabisa. Kwa hivyo miguu yao ni mirefu yenye makucha makali ili kushikilia mawe ndani ya maji matiririkayo. Pia hutumia mabawa yao mafupi kama aina za mapezi. Hula lava na viluwiluwi vya wadudu wa maji hasa lakini samaki wadogo, mayai ya samaki, makoa na gegereka pia. Tago lao kubwa hujengwa kwa vigoga karibu na maji katika shimo lo lote au chini ya daraja. Jike huyataga mayai 2-4.
Spishi ya Afrika
- Cinclus cinclus, Mkesha-maji (White-throated Dipper)
- Cinclus c. minor, Mkesha-maji Kaskazi (Northwest African Dipper)
Spishi za mabara mengine
- Cinclus leucocephalus (White-capped Dipper)
- Cinclus mexicanus (American Dipper)
- Cinclus pallasii (Brown Dipper)
- Cinclus schulzi (Rufous-throated Dipper)
Picha
- Mkesha-maji wa Ulaya
- White-capped dipper
- American dipper
- Brown dipper
- Brown dipper, mchanga katika maji
- Rufous-throated dipper
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoAina za manenoKumaShairiKamusi za KiswahiliDiamond PlatnumzMaumivu ya kiunoInsha ya wasifuSimba S.C.Fasihi simuliziIdd el HajjTanzaniaOrodha ya Watakatifu WakristoHifadhi ya mazingiraMikoa ya TanzaniaMaalum:MabadalikoyaKaribuniKisaweNembo ya TanzaniaMapenziJohn Raphael BoccoMapenzi ya jinsia mojaTendo la ndoaVivumishiUandishi wa ripotiOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaMazingiraMpira wa miguuMshororoVitendawiliOrodha ya makabila ya TanzaniaMadawa ya kulevyaMasoud KipanyaKiswahiliNahauMofimuVita Kuu ya Pili ya Dunia