Ghuba ya Saint Lawrence
48°0′N 61°30′W / 48.000°N 61.500°W
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/ce/Golfe_Saint-Laurent_en.png/300px-Golfe_Saint-Laurent_en.png)
Ghuba ya Saint Lawrence (kwa Kiingereza: Gulf of Saint Lawrence, kwa Kifaransa. golfe du Saint-Laurent) ni eneo la mdomo wa Mto Saint Lawrence katika Bahari Atlantiki. Hivyo ni pia sehemu ambako maji ya maziwa makubwa ya Amerika Kaskazini yanaishia baharini. Mkono huu wa bahari umefungwa na nchi kavu ya Kanada pande tatu na una eneo la maji la km2 236,000.
Jiografia
Ghuba hiyo inapakana upande wa kaskazini na Rasi ya Labrador, upande wa mashariki na Newfoundland, upande wa kusini na Nova Scotia na upande wa magharibi na Rasi Gaspé na New Brunswick.
Kuna milango miwili ambako ghuba inaunganishwa na Atlantiki:
- Mlangobahari wa Belle Isle baina ya Labrador na Newfoundland (una upana wa km 17 na kina cha m 60).
- Mlangobahari wa Cabot baina ya Newfoundland na Kisiwa cha Cape Breton (una upana wa km 104 na kina cha m 480).
Tanbihi
Viungo vya Nje
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoAina za manenoKumaShairiKamusi za KiswahiliDiamond PlatnumzMaumivu ya kiunoInsha ya wasifuSimba S.C.Fasihi simuliziIdd el HajjTanzaniaOrodha ya Watakatifu WakristoHifadhi ya mazingiraMikoa ya TanzaniaMaalum:MabadalikoyaKaribuniKisaweNembo ya TanzaniaMapenziJohn Raphael BoccoMapenzi ya jinsia mojaTendo la ndoaVivumishiUandishi wa ripotiOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaMazingiraMpira wa miguuMshororoVitendawiliOrodha ya makabila ya TanzaniaMadawa ya kulevyaMasoud KipanyaKiswahiliNahauMofimuVita Kuu ya Pili ya Dunia