Alfa na Omega
Alfa (Α au α) na omega (Ω or ω) ndizo herufi ya kwanza na ya mwisho ya alfabeti ya Kigiriki.
Kwa sababu hiyo zimechukuliwa kama ishara ya mwanzo na mwisho.
Kitabu cha Ufunuo (1:8, 21:6 na 22:13)[1] kinazitumia pamoja kama jina la Yesu Kristo na la Mungu[2][3], kwa kuwa ndio asili na kikomo cha viumbe vyote.
Picha
- Alfa na omega kandokando ya mchoro wa Yesu, karne ya 4
- "ΑΩ" katika kioo cha rangi
- Ishara nyingine ya Kristo pamoja na Alfa na Omega
Katika Uyahudi
Maandishi ya Uyahudi yanasema kuwa neno emet (אמת, yaani "uaminifu"), moja ya sifa kuu za YHWH, linaundwa na herufi ya kwanza, ya kati na ya mwisho wa alfabeti ya Kiebrania.
Katika Uislamu
Qur'an (57:3) inataja al'Awwal (الأول), yaani "Wa Kwanza" na al'Akhir (الآخر), yaani "Wa Mwisho" kati ya majina ya Allah.
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
- Hassett, Maurice M. (1907). "A and Ω". Catholic Encyclopedia. 1. New York: Robert Appleton Company.
- "Alpha and Omega (in Scripture)" in the Catholic Encyclopedia at newadvent.org
- "Alpha and Omega" at the Jewish Encyclopedia
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Alfa na Omega kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoAina za manenoKumaShairiKamusi za KiswahiliDiamond PlatnumzMaumivu ya kiunoInsha ya wasifuSimba S.C.Fasihi simuliziIdd el HajjTanzaniaOrodha ya Watakatifu WakristoHifadhi ya mazingiraMikoa ya TanzaniaMaalum:MabadalikoyaKaribuniKisaweNembo ya TanzaniaMapenziJohn Raphael BoccoMapenzi ya jinsia mojaTendo la ndoaVivumishiUandishi wa ripotiOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaMazingiraMpira wa miguuMshororoVitendawiliOrodha ya makabila ya TanzaniaMadawa ya kulevyaMasoud KipanyaKiswahiliNahauMofimuVita Kuu ya Pili ya Dunia